
Mtakatifu Brigita alizaliwa nchini Ireland mnamo mwaka 451 na alifariki mwaka 525 japo vyanzo vingine vinaonesha kuwa alizaliwa mwaka 453 na kufariki mwaka 524.Ukisoma baadhi ya vyanzo vingine inaonesha palikuwepo mjadala ambao ulikuwa ukizungumziwa kuhusu wazazi wake ila kwa ukubwa inasemekana mama yake alikuwa anaitwa Brocca ambaye alikuwa mtumwa kwa mantiki hiyo Mtakatifu Brigita alizaliwa ndani ya Utumwa.
Mtakatifu Brigita aliweza kupata ubatizo wake ambao alibatizwa na Mtakatifu Patriki na Baba yake alikuwa anaitwa Dubthach.Mtakatifu Brigita ni mjawapo wa msimamizi wa nchi ya Ireland pamoja na Mtakatifu Patricki na Mtakatifu Kolumba.
Mtakatifu Brigita wa Ireland kadri ya maandiko inasemekana alikuwa mmonaki abesi mwanzili wa monasteri mbalimbali za kike, ikiwemo ile maarufu ya Kildare nchini Ireland.Mtakatifu huyu inasemekana alitoa mchango mkubwa katika uinjilishaji kwenye hicho kisiwa mpaka leo unamchango mkubwa kiimani. Na hivyo anahesabika Anahesabiwa na madhehebu mbalimbali ya Kikristo ambayo ni Wakatoliki,Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.
Sikukuu yake huazimishwa kila mwaka Februari mosi(1 February) pamoja na ya Mtakatifu Dar Lugdach ambaye alikuwa mwanafunzi wake aliyekuwa amerithi mamlaka yake.
kwa kusoma zaidi bonyeza hapa:
No comments:
Post a Comment