Wednesday, November 15, 2017

Maisha ya Mtakatifu Albeto

Related image
Mtakatifu Alberto Mkuu alizaliwa nchini Ujerumani mwaka 1205 na alifariki tarehe 15 Novemba 1280.  Jina Alberto alilopewa kwa heshima askofu  Alberto wa Bollstädt (au wa Cologne) kutokana na mchango wake mkubwa upande wa elimu alioutoa   na ule wa dini  na vilevile upande wa uchungaji na wa upatanishi wa watu na watawala.
Mtakatifu Alberto alikuwa  Mtawa wa  Shirika la Wahubiri, anahesabiwa kuwa mwanafalsafa  na mwanateologia  bora wa Ujerumani  katika Karne ya Kati .
Mtakatifu Alberto Alijitahidi kulinganisha imani  na akili akiingiza falsafa  ya Aristotle  katika Ukristo, jambo lililoendelezwa na mwanafunzi wake bora,Mtakatifu Thomasi wa Akwino.
Alitangazwa na Papa Gregori XV kuwa Mwenyeheri  mwaka 1622 na baadae alitangazwa kuwa Mtakatifu Na Mwalimu wa Kanisa na Papa Pius XI, tarehe 16 Desemba 1931.Mwaka 1941 Papa Pius XII  alimtangaza msimamizi wa wanasayansi .
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 15 Novemba.

No comments:

Post a Comment